RIDHIWANI KIKWETE AMEDAI HABEBWI NA BABA YAKE, RAIS JAKAYA KIKWETE

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiv_0O-0Vre3T9RIyUneNRFcosG4tRm5IaX7mgxRPeiNNfsFsMhBf51Kii-MfKhjlpKQepQh2WIaKidnLlQIcjQjdw5tRxHGTnu7SejTD5bDnCHxHuQTvkX7gdY1uVZg-i7lCIy1oRsuYk/s640/RidhiwaniKikwete.jpg

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), wilayani Bagamoyo, anayetarajiwa kuwania ubunge Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete, amesema habebwi na baba yake, Rais Jakaya Kikwete, katika harakati zake za kisiasa.

Ridhiwani aliyasema hayo alipozungumza na waandishi wa habari juzi jioni baada ya kutangazwa kwa matokeo ya kura za maoni katika jimbo hilo kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Msata.

Alisema anafanya siasa bila kupitia mgongo wa baba yake, Rais Kikwete.

“Siasa ninayofanya haina mahusiano na baba yangu, nafanya siasa kwa maisha yangu na sina ubia na baba yangu katika hili,” alisisitiza.

Akijibu swali la kwanini amejiingiza katika siasa tofauti na maneno yake mwaka 2010 kuwa hawezi kushiriki katika kinyang’anyiro cha ubunge kwenye jimbo hilo, Ridhiwani alisema hakuwa tayari kujitangaza kwa kipindi hicho ili kutowapa nafasi maadui kutawala kabla ya wakati.

Aidha, Ridhiwani aliomba mshikamano na ushirikiano kwa wana-CCM kufanikisha azima ya kutetea jimbo hilo katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwezi ujao.

Katika kura za maoni, Ridhiwani alipata kura 758, Imani Madega, kura 335, Maneno kura 206 na mwanamke pekee aliyeshiriki katika mchakato huo, Mkwazu Changwa, alipata kura 17.

Kamati Kuu (CC) ya CCM inatarajia kukutana Machi 8, mwaka huu  kupitisha jina moja litakaloshiriki kumpata mbunge wa Jimbo la Chalinze kufuatia kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Said Bwanamdogo.
 
CHANZO: NIPASHE

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

Post a Comment

Ungana Nasi, Like Page Yetu Hapa Chini