Showing posts with label KIMATAIFA. Show all posts
Showing posts with label KIMATAIFA. Show all posts

PRESIDENT KIKWETE IN BILATERAL TALKS WITH PRESIDENT OF THE EUROPEAN COMMISSION BARROSO


President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete meets the President of the European Commission Jose Manuel Barroso at his Office in Brussels Belgium this morning. President Kikwete was in Brussels where he attended the 4th EU Africa Summit under the theme, ”Investing in People, prosperity and peace”.

Soma Habari Kamili

FAHAMU KUHUSU NDEGE YA MALAYSIA ILIYOPOTEA


Ndege ya shirika la ndege la Malaysia (Malaysia Airlines). 
Kuna mambo ambayo watu hawajafahamishwa kuhusu ndege ya shirika la ndege la Malaysia (Malaysia Airlines) safari namba Flight 370 ambayo imepotea ikiwa eneo la juu ya bahari katika Ghuba ya Thailand na watu 239. 
Ndege hiyo aina ya Boeing 777 iliyopotea Jumamosi asubuhi wiki iliyopita na kutoonekana mpaka leo imewababaisha wataalam wengi duniani wa mambo ya usalama wa vyombo vya anga. 
Muonekano wa ndani wa Ndege ya shirika la ndege la Malaysia. 
Hata hivyo, pamoja na mkanganyiko huo, gazeti la Wall Street Journal limeorodhesha mambo ambayo watu wengi hawayafahamu kuhusiana na kupotea kwa ndege hiyo. SOMA ZAIDI
Mambo hayo ni yafuatayo: 
Ndege zote za Boeing 777 zina kisanduku maalum cha kutunza kumbukumbu za mawasiliano ya marubani wa ndege na waongoza ndege walioko ardhini (black box) ambacho hakiwezi kuharibika katika mlipuko wowote unaoweza kutokea kwenye ndege.
Kijisanduku hicho (black box) kina nguvu za kurusha mawimbi kuonyesha kilipo kwa siku zisizopungua 30 baada ya kuanguka baharini. 
Hata hivyo, wataalam wameshindwa kunasa mawimbi ya chombo hicho na hivyo kuwa na wasiwasi kwamba huenda kimeharibiwa na nguvu kubwa isyokuwa ya kawaida. 
Sehemu nyingi zilizoharibika za ndege huwa zinaelea juu ya maji baada ya ndege kuanguka baharini au majini. 
Katika tukio hili hakuna kilichoonekana, na hivyo kuzua hofu kwamba ndege hiyo huenda imetoweka katika eneo la Dunia. 
Iwapo kombora lingeipiga ndege hiyo, basi kombora hilo lingeonekana katika vyombo vya uchunguzi vya kijeshi na vya usalama wa safari za anga. Hii ni pamoja na kwamba huenda imepigwa na kombora na kuikatakata ndege hiyo katika vipande vidogo-vidogo. 
Katika nadharia hii, hakuna dalili zozote zilizonaswa na vyombo vya ulinzi na usalama kuonyesha kulikuwa na kombora lililohusika. 
Pamoja na eneo ambalo ndege hiyo ilikata mawasiliano na kupotea kufahamika, bado wataalam wameshindwa kujua iko wapi. 
Kufahamu eneo la tukio, mwelekeo na kasi ya ndege hiyo, bado hakujasaidia kupatikana kwa ndege hiyo, hivyo kuzidisha hofu inayowachanganya wataalam. 
Iwapo Flight 370 ilitekwa, isingeacha kuonekana kwenye vyombo vya kudadisia nyendo za vyombo vya angani (radar). 
Nadharia ya kutekwa haina msingi wowote, kwani ndege zinazotekwa huwa hazitoweki katika radar. 


HITIMISHO: Ndege hiyo ya Boeing 777 haikulipuka angani, bali imetoweka!

Soma Habari Kamili

KAMA IKITHIBITIKA; JACK PATRICK JELA MIAKA 10!

Jack.

Duh! Habari mpya kutoka huko Hong Kong, China zinaeleza kuwa kama atapatikana na hatia ya kukamatwa na madawa ya kulevya ‘unga’, modo maarufu Bongo, Jacqueline Fitzpatrick Cliff ‘Jack Patrick’ atatumikia kifungo cha miaka kumi jela.

Kwa mujibu wa chanzo makini ambacho kilikwenda kumtembelea Jack akiwa nyuma ya nondo baada ya kuruhusiwa kumuona tangu Machi mosi, mwaka huu, mwanamitindo huyo amekata tamaa na hana matumaini ya kutoka jela hivi karibuni.
“Aisee Jack Cliff anatia huruma sana, hana matumaini ya kutoka hivi karibuni na ana maumivu ya kupitiliza,” kilisema chanzo hicho.
Jack Patrick akiwa akiwa mikononi mwa polisi nchini China baada ya kukutwa na pipi za heroin tumboni.
Mpashaji huyo alizidi kuweka wazi kuwa Jack anasema kuwa kesi yake ni ngumu na endapo atapatikana na hatia, basi atakumbana na kifungo, si chini ya miaka kumi, jambo ambalo limemfanya kudondosha machozi kila kukicha huku akituma salamu nyumbani kwao Bongo.
Jack alikamatwa na unga kilo 1.1 huko Macau, Hong Kong mwezi Desemba, mwaka jana ambapo sasa kesi yake itaanza kuunguruma Septemba, mwaka huu.

Soma Habari Kamili

KWA MUJIBU WA RIPOTI YA SHIRIKA LA KIJASUSI LA MAREKANI ( CIA ) , TANZANIA NI NCHI YA 12 KIUCHUMI BARANI AFRIKA, KIDUNIA NI YA 83!

Kwa mujibu wa ripoti ya shirika la kijasusi la Marekani, CIA iitwayo The World Fact Book, Tanzania ni nchi ya 12 kiuchumi barani Afrika na 83 duniani.

Soma Habari Kamili

TELEX FREE YACHUNGUZWA NCHINI RWANDA

The government is investigating the operations of a business that has attracted many Rwandans with its quick cashback philosophy, typical of pyramid schemes also known as Ponzi schemes.
TelexFREE, an Internet-based service, requires new members to pay more than $1,570 (Rwf1,067,600) and post three advertisement links to start earning $100 (Rwf68,045.26) weekly. By recruiting new members, one stands to earn bonuses, it claims.
TelexFREE has been banned in Brazil and is under investigation in the US and other countries around the world on suspicions that it could be a Ponzi scheme.
Emmanuel Bayingana, the official in charge of Competition at the Ministry of Trade and Industry, confirmed that TelexFREE was being investigated.
“We are doing an assessment of the operations of TelexFREE,” Mr Bayingana said. “The investigations will determine the way forward. The assessment will be concluded next week.”
He noted that the ministry, Rwanda Development Board (RDB) and the central bank will come up with a position, especially if the business is found to be risk-prone.
The government has been strict on pyramid schemes and multi-level marketing businesses with a number of them, including Questnet, banned from operating in Rwanda.
At the TelexFREE offices in the Kigali suburb of Remera near the taxi park in a new complex that also houses Bank of Kigali, a few office staff members lurk around trying to win more clients.
“It’s a profitable business. You can join and make $100 a week. I make the same every week by just posting three links,” one of the staff members only identified as Hakim said in an attempt to convince the writer to join the scheme.
TelexFREE is a multi-level Internet marketing scheme which uses VoIP technology to share advertisements online. Fred Ndoli, one of the members and an active recruiter, maintains that the business is genuine.
Recoup investment
“People are making money,” Mr Ndoli said. “I earn $100 a week after investing in it. I post links from a computer or using my phone. It takes only five minutes.”
Mr Ndoli said he only joined two months ago but was confident he would recoup his investment and make even more money soon. He insisted that those crying foul failed to fulfil their part of the agreement.
“I think they failed to post links,” he said. “You make money by posting links. If you don’t post links, you don’t make money.”
Three people who lost their savings in the scheme told Rwanda Today they were told that they failed to “post links” to recover their money.

One of them, who joined recently, said he was informed that once one fails to post links they forfeit their investment.“It’s a risky business. It means that you have to have Internet everyday, wherever you are, because if you fail to post you lose your money,” the member said on condition of anonymity.
Efforts to reach the country director of TelexFREE, Fred Nyakana, were futile as calls and messages to his phone went unanswered. When we visited the offices, Mr Nyakana was said to be in a meeting.
Many members say they are making money but experts in such multi-level marketing businesses contend that those who join first make money while those who join later “only pay those who recruited them.”
According to Ted Nuyten, an international home-business marketing expert, such schemes usually collapse after more people join. When the business starts becoming passive and stagnated, the founders pull out, leaving hundreds, if not thousands, of complainants behind.
In a review Mr Nuyten did for TelexFREE, he does not recommend people to join the scheme basing on some facts around the said business. He says the fact that it was banned in Brazil qualifies it as a Ponzi scheme.
“In fact, in Brazil, TelexFree has been shut down since June of 2013, its assets frozen, they have been ordered not to recruit any new people in the country and they not to pay any commissions and bonuses,” Mr Nuyten noted.
“They have lost a number of appeals to have the injunction against them lifted, not to mention that they have been fined for not meeting the various requirements in Brazil to operate as a VoIP company.”
He added that TelexFREE was under criminal investigation in Brazil after it diverted its earnings, amounting $88 million (Rwf61 billion), to secret accounts to avoid legal action and that in the United States regulatory bodies were closely watching the Brazil situation.
“Anyone involved with TelexFREE is either new to the industry and/or knows nothing about regulatory compliance as it relates to a network marketing company and opportunity,” he said. “TelexFREE is a very high-risk investment opportunity.”
Mr Nuyten also pointed out that the fact that somebody was making money did not make the scheme legal or legitimate.

Soma Habari Kamili

FACEBOOK, INSTAGRAM NA WHATSAPP KUSITISHA KUTOA HUDUMA NCHINI UGANDA BAADA YA RAIS WA NCHI HIYO YOWERI MUSEVENI KUPINGA SHERIA YA KUZUIA USHOGA


Ikiwi ni siku chache baada ya Rais Yoweri Museveni wa Uganda kusaini muswaada wa sheria ya kupinga ushoga nchini humo, kampuni ya Facebook imetangaza uwezekano wa kusitisha huduma zake nchini Uganda kama njia ya kupinga uamuzi huo ambao wamedai kuwa unakiuka haki za baadhi ya watu.
 
Taarifa iliyotolewa na kampuni hiyo inasema kuwa, Facebook ilianzishwa kusupport haki za binadamu kwa kuwapa nafasi watu wote ya kujielezea kwa uhuru, hivyo wanasikitishwa kujua kwamba Uganda kama nchi imesaini muswaada wa sheria ya kupinga ushoga.
 
Taarifa hiyo inaendelea kusema Facebook kwa sasa inatazama upya juu ya kujihusisha kwake kutoa huduma nchini Uganda, na kuongeza kuwa kusitisha kutoa huduma zake za Facebook, Instagram na Whatsapp nchini humo kwa muda watakaoona unafaa, ni moja ya hatua wanayofikiria kuchukua kama njia ya kuonesha kutoridhishwa kwao na uamuzi huo.
Isome taarifa hiyo:

STATEMENT FROM FACEBOOK ON ANTI-HOMOS6XU8LITY LAW
 
When we launched Facebook, we thought it as a platform to advance people’s rights and liberties of self expression in all form. We were equally shocked to learn that Uganda as a country had gone ahead to sign the Anti Homos9xu9lity bill into a law.

Facebook is currently reviewing its engagement to Uganda, as we seek to come up with a voice to express our dissatisfaction. And of course, suspending our operations in Uganda is one of the options we are considering. In the event that we suspend operations in Uganda, our platforms of Instagram, Facebook and Whatsapp will be off for a time we shall deem necessary.

We strongly condemn the act of the Ugandan Government to overstep the rights of a minority. All humans are created equal and deserve a right to freedom and happiness.
Signed
Sheryl Kara Sandberg
Chief Operations Officer (COO) At Facebook
 
Mmoja wa wamiliki wenza wa Facebook, Chris Hughes ni shoga na aliolewa na June 30, 2012 na mwanaume mwenzake, Sean Eldridge.
 ******
(Kwa  hisani ya  Bongo5 )

Soma Habari Kamili

BENKI YA DUNIA YABANA MISAADA KWA UGANDA IKIWA NI SIKU CHACHE TU BAADA YA RAIS YOWERI MUSEVENI KUIDHINISHA SHERIA MPYA DHIDI YA USHOGA


Benki ya dunia imebana msaada wa dola milioni 90 kwa Uganda , siku chache tu baada ya Rais Yoweri Museveni kuidhinisha sheria mpya dhidi ya mapenzi ya jinsia moja.
 
Sheria iliyoidhinishwa na Rais Yoweri Museveni, ilitiwa saini Jumatatu na inatoa adhabu kali kwa watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja.
 
Wafadhili wengine tayari wameanza kusitisha misaada Uganda. Wahisani kama Denmark na Norway wamesema kuwa wataanza kufadhili mashirika moja kwa moja badala ya serikali.
 
Asilimia 20% ya bajeti ya Uganda inategemea michango ya wafadhili.
 
Mpaka sasa nchi tatu za Ulaya zimeamua kukata misaada yao kwa mamilioni ya dola.
 
Wizara ya fedha ya Uganda imesema inasubiri mawasiliano rasmi ya nchi husika, na iko tayari kukabiliana na athari za hatua hiyo.
 
Hadi kufikia sasa Waziri wa Fedha Wa Sweden, akiwa mjini Kampala, alisema wawekezaji kutoka nchi yake watakuwa na wakati mgumu kuweka pesa zao nchini Uganda kwa sababu watakuwa na hofu kuwa sheria yoyote inaweza kupitishwa kuwadhulumu watu.
 
Jana serikali ya Uholanzi ilisema itazuia kwa muda misaada kwa Serikali ya Uganda. Norway na Denmark pia zimetangaza kupunguza au kusimamisha kwa muda misaada yake kwa Uganda.

>>BBC Swahili

Soma Habari Kamili

WAISLAM WENYE ITIKADI KALI WAHUKUMIWA JELA KIFUNGO CHA MAISHA KWA KUUA NCHINI UINGEREZA


Gemini Donnelly-Martin, 20, na mama yake Amanda (kulia) wakiongea na Adebolajo wakati Ingrid Loyau-Kennett (kushoto) akiongea na Adebowale. Pembeni kushoto ni mwili wa Lee Rigby baada ya kuuawa.

Lee Rigby enzi za uhai wake akiwa na mpenzi wake Aimee West.
Magari  yakiwapeleka wafungwa hao gerezani.
Mtoto pekee wa marehemu.
Waandamanaji wakiwa nje ya mahakama wakati wa hukumu hiyo.
 
Michael Adebolajo.

 
Michael Adebowale.

 
Marehemu Lee Rigby.
WAISLAM wawili wenye itikadi kali nchini Uingereza, Michael Adebolajo na Michael Adebowale walitiwa hatiani Desemba mwaka jana na kuhukumiwa vifungo virefu kwa mauaji ya Lee Rigby huko Woolwich Barracks, kusini-mashariki mwa jiji la London mnamo Mei mwaka jana.
Waingereza hao weusi waliozaliwa nchini humo, walihukumiwa majuzi katika mahakama ya Old Bailey ambako walianzisha vurugu baada ya hukumu hiyo kwa kupiga kelele za  'Allahu akbar'  (Mungu Mkubwa) huku wakiwashambulia askari wa magereza.
Adebolajo (29) alihukumiwa kifungo cha maisha na Adebowale (22) amehukumiwa kifungo cha miaka 45 ikiwa na maana atatoka gerezani akiwa na umri wa miaka 67.
Watu hao walimshambulia Rigby wakati akitembea mtaani na  kumkatakata kwa silaha  hadi kufa, yote hayo yakifanyika mbele ya watu waliokuwa wamepigwa butwaa.
Washambuliaji hao walidai kuwa walikuwa ‘askari wa Mungu’ na walifanya hivyo kutokana na matatizo wanayoyapata Waislam wengine walio nchi za nje na kwamba walikuwa hawajutii kitendo hicho.
Kutokana na vurugu zao walizofanya mahakamani kwa kumrushia maneno hakimu, askari waliwatoa nje na hivyo hukumu yao kutolewa wakiwa hawamo mahakamani.
Miongoni mwa maneno waliyoyasema ni: “Wewe (Uingereza) na Marekani kamwe hamtakuwa salama.”

(DAILY MAIL)

Soma Habari Kamili

TETESI: WAMILIKI WA FACEBOOK NA INSTAGRAM WAIFUNGIA UGANDA ILI KUMKOMESHA YOWERI MUSEVENI BAADA YA KUPINGA USHOGA NCHINI HUMO

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhdcQU6rHRMCfEWb2TEO3jpPAzr4-GDXaqb4h_Sz7Ezz-4CqpKl4exqahVqR_K09OjtTkzzJPdHHqOqMWcUoI5bMQpxl13vTJ-I21by_O4Xw14rbv_S5xTTeSiSENkG0FchS3qqs11W81iI/s640/museven.jpg
Kufuatia Rais wa Uganda kusaini sheria mpya ya kupinga Ushoga na aina zote za namna hiyo, wamiliki wa Facebook, Instagram, na Twitter wamefunga huduma zote katika nchi ya Uganda ikiwa ni ishara ya kuonyesha kutoridhishwa kwao na hatua ya Museven kusaini sheria hiyo. Kwa sasa wananchi wa Uganda hawatapata huduma hizi labda Rais wao aamue vinginevyo katika sheria hiyo.

Soma Habari Kamili

SHEREHE YA AINA YAKE YAFANYIKA NCHINI INDONESIA...WAFU WAFUFULIWA LAIVU!

corpse-new-clothes
wafu
Kuna makabila na tamaduni nyingi nchini Indonesia, lakini hii ni tamaduni ya kipekee, ya kushangaza na kuogopesha. Tamaduni hii hujulikana kama sherehe ya kufufua wafu na kuwapeleka kwenye makazi yao ya kudumu.
Watu wa Toraja, Indonesia huamini kuwa mtu anapokufa huanza safari ndefu kuelekea kwenye hatima yake, hivyo kuna vitu ambavyo lazima vifanyike kumsaidia kwenda na kufika salama, ambavyo huhusisha gharama kubwa. Kutokana na gharama kubwa za mazishi hayo, jamii nyingi hulazimika kuzika wafu wao katika majeneza ya muda, mpaka baada ya zoezi la kukusanya pesa kwa aliji ya shughuli ya mazishi kukamilika.
Kwakua ardhi kubwa ya maeneo ya Toraja ni milima, na hivyo kufanya zoezi la kuwabeba wafu hao kuwa gumu, jamii huamini kuwa wafu hao huweza kwenda wenyewe kwa kutembea kwa miguu wakisindikizwa na ndugu zao. Baada ya kufika kwenye makazi yao, inasadikika kuwa wanakufa tena, ndugu zao huwaosha na kuwavalisha nguo mpya na kisha kuwazika tena.
Kwa siku za hivi karibuni, tamaduni hii imeanza kupotea kwa wakazi wengi, japo kwa watu wachache wanaoaminiwa na wazee wao kwamba wanaweza kurithi tamaduni hii, bado wanaifanya

Soma Habari Kamili

HUYU NDIYE MTANZANIA ALIYEBAKWA NCHINI CHINA MPAKA KUFA, MAITI YAKUTWA HAINA FIGO WALA MOYO!

 
Sabrina au Habiba enzi za uhai wake.
AMA kweli dunia hadaa, ulimwengu shujaa! Kumeibuka mchezo mchafu, kuna Watanzania wanawachukua warembo nchini na kuwapeleka China kwa ahadi kwamba wanakwenda kufanya kazi saluni, wakifika kule wanawanyang’anya paspoti na kuwauza kwa wanaume (ukahaba), sasa yamemkuta Mbongo aitwaye Sabrina au Habiba, Ijumaa Wikienda lina mkasa wa kusikitisha.
Habari za uhakika kutoka kwa chanzo chetu nchini humo zilisema kuwa, Sabrina (24), alifariki dunia Alhamisi iliyopita kufuatia kubakwa na wanaume watano, raia wa Nigeria ambao wamo nchini humo kibiashara.
Tukio hilo lilijiri kwenye hoteli moja iliyopo kwenye Mji wa Guangzhou ambao umejaa wageni wengi, wakiwemo Watanzania.
SIKU YA TUKIO
Rafiki wa karibu wa Sabrina, Saada alisema siku ya tukio, marehemu akiwa katika harakati zake za kutafuta wateja alikutana na Mnigeria mmoja ambaye walipatana kulala wote kwa usiku mzima.
“Kumbe yule Mnaigeria alikuwa na wenzake wanne. Usiku walimwingilia wote kwa nguvu kwa kumbaka mpaka akapoteza maisha palepale. Ni ukatili mkubwa.
 
“Wale watu walipogundua Sabrina amekufa waliuchukua mwili wake na kuutupa chini kutoka ghorofa ya tano,” alisema rafiki huyo.

MAITI YAKUTWA HAINA FIGO, MOYO
Habari zaidi zilidai kuwa mpaka juzi (Jumamosi) madaktari waliokuwa wakiuchunguza mwili wa Sabrina waligundua hauna figo na moyo, jambo linalozidi kuzua hofu juu ya muaji yake.

NI BIASHARA ILIYOIBUKA CHINA?
Ilidaiwa kuwa nchini China imeibuka biashara ya viungo mbalimbali vya binadamu ambapo ili vipatikane ni lazima mwenye viungo hivyo auawe kwa njia yoyote.

SABRINA AFA, MGANDA APOTEA
Mtoa habari wetu alisema wakati Wabongo wakiwa kwenye maombolezo ya kifo cha Mtanzania huyo, mrembo mwingine raia wa Uganda, nchi ambayo imo ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki amepotea katika mazingira ya kutatanisha nchini humo.
Baadhi ya watu wana wasiwasi kuwa kupotea kwa msichana huyo kunahusiana na kushamiri kwa biashara ya viungo vya binadamu.

SABRINA ALIKWENDAJE CHINA?
Mwezi Julai, mwaka jana, Sabrina alikwenda nchini humo akidanganywa na mwanamke mmoja kwamba atapata kazi kwenye saluni ya wanawake lakini baada ya kufika alijikuta akiingizwa kwenye biashara ya ukahaba bila ridhaa yake mpaka alipokutwa na mkasa huo uliopoteza maisha yake.

TAHADHARI KWA WAREMBO WANAOKWENDA CHINA KUFANYA KAZI SALUNI
Imebainika kuwa, kumeibuka wimbi la Wabongo wanaofanya ‘uwakala’ wa kuwachukua wasichana wa Kitanzania kwa kuwadanganya kwamba wanakwenda kufanya kazi za saluni nchini humo.
Mara baada ya kufika, wasichana hao hunyang’anywa paspoti ili washindwe kuondoka nchini humo na kushinikizwa kujiuza (ukahaba) huku waliowapeleka wakipokea fedha kutoka kwa wateja.

KUIKOMBOA PASPOTI
Habari zilisema kuwa mhusika hurejeshewa paspoti yake baada ya malipo yake kwa ‘wakala’ kufikia dola za Marekani 8,000 (kama shilingi milioni 12), ndipo huachiwa ‘huru’ kuendelea na maisha yake.
Wengi wakishaachiwa hushindwa kurejea Bongo na kujikuta wakiendelea kuuza miili katika mahoteli na klabu huku wakikutana na majanga mbalimbali.

MASOGANGE, KAJALA NA DIDA
Watanzania waishio nchini humo wamewatahadharisha mastaa wa Bongo, wakiwemo Mtangazaji wa Radio TimesFM, Khadija Shaibu ‘Dida’, msanii wa filamu Kajala Masanja na Video Queen Agnes Gerald ‘Masogange’ ambao hupenda kwenda nchini humo kwa shughuli zao, kutokubali kuwa karibu na mawakala wa kuchukua wasichana Bongo kwa kuwadanganyia kazi ya saluni kwani wanaweza kujikuta pabaya siku moja.

DIDA
Ijumaa Wikienda lilimsaka Dida siku ya Jumamosi iliyopita na kumuuliza kuhusu kuwepo kwa mawakala hao ambapo alikiri kusikia huku akisema warembo wenyewe wanapaswa kuwa macho na udanganyifu huo.
“Najua wapo Wabongo wanaofanya shughuli hiyo, si China tu hata India, unapelekwa kwa ahadi ya kazi ya saluni, ukifika hamna cha saluni wala nini? Warembo wawe makini jamani, nenda China kama una uwezo wako mwenyewe kufanya ‘shoping’ lakini si kupelekwa,” alisema Dida.

BALOZI WA TANZANIA-CHINA
Juzi, Ijumaa Wikienda lilimtafuta Balozi wa Tanzania nchini China, Luteni Jenerali Mstaafu Abdulrahman Shimbo ili azungumze lolote kuhusu tukio la Sabrina, lakini simu yake ilionekana kutokuwa hewani kwa muda mrefu.

Soma Habari Kamili

RAIS WA UGANDA YOWERI MUSEVENI AMKASHIFU OBAMA KUHUSU KURUHUSU USHOGA UGANDA

Raisi Yoweri Museveni.
Rais Yoweri Museveni wa Uganda ametoa matamshi makali dhidi ya Rais Barack Obama wa Marekani akimtaka akome kungilia masuala ya ndani ya Uganda.

Matamshi hayo makali yamekuja baada ya Rais wa Marekani kutishia kuwa uhusiano wa nchi yake na Uganda utaharibika iwapo Rais Museveni atasaini na kuufanya kuwa sheria muswada wa kupinga vitendo vichafu vya kujamiiana watu wa jinsia moja.

Agusia Kushirikiana na Russia.
Rais Museveni amesema, atashirikiana na Russia iwapo Marekani itaendelea kuingilia masuala ya ndani ya Uganda na kuongeza kama ninavyomnukuu:

“Russia imekuwa ikifanya shughuli zake barani Afrika tangu mwaka 1917 yaani kwa zaidi ya miaka 100. Ninataka kushirikiana na Russia kwa sababu hawachanganyi siasa zao na siasa za nchi nyingine.” Mwisho wa kunukuu

Ameongeza kuwa: “Ukiona mtu anaingia ndani ya nyumba ya mtu mwingine basi jua kuna tatizo. Hapa ni nyumbani petu. Huwezi kumuona mtu mwenye upaa kama mimi hivi ndani ya nyumba yake na kuanza kumpangia afanye unavyotaka wewe. Rudi kwenu!” Alisema Rais Museveni

Soma Habari Kamili

MWANAMKE WA KITANZANIA ABAKWA NCHINI CHINA MPAKA KUFA



AMA kweli dunia hadaa, ulimwengu shujaa! Kumeibuka mchezo mchafu, kuna Watanzania wanawachukua warembo nchini na kuwapeleka China kwa ahadi kwamba wanakwenda kufanya kazi saluni, wakifika kule wanawanyang’anya paspoti na kuwauza kwa wanaume (ukahaba), sasa yamemkuta Mbongo aitwaye Sabrina au Habiba, Ijumaa Wikienda lina mkasa wa kusikitisha.
Habari za uhakika kutoka kwa chanzo chetu nchini humo zilisema kuwa, Sabrina (24), alifariki dunia Alhamisi iliyopita kufuatia kubakwa na wanaume watano, raia wa Nigeria ambao wamo nchini humo kibiashara.
Tukio hilo lilijiri kwenye hoteli moja iliyopo kwenye Mji wa Guangzhou ambao umejaa wageni wengi, wakiwemo Watanzania.

SIKU YA TUKIO
Rafiki wa karibu wa Sabrina, Saada alisema siku ya tukio, marehemu akiwa katika harakati zake za kutafuta wateja alikutana na Mnigeria mmoja ambaye walipatana kulala wote kwa usiku mzima.
“Kumbe yule Mnaigeria alikuwa na wenzake wanne. Usiku walimwingilia wote kwa nguvu kwa kumbaka mpaka akapoteza maisha palepale. Ni ukatili mkubwa.
“Wale watu walipogundua Sabrina amekufa waliuchukua mwili wake na kuutupa chini kutoka ghorofa ya tano,” alisema rafiki huyo.

MAITI YAKUTWA HAINA FIGO, MOYO
Habari zaidi zilidai kuwa mpaka juzi (Jumamosi) madaktari waliokuwa wakiuchunguza mwili wa Sabrina waligundua hauna figo na moyo, jambo linalozidi kuzua hofu juu ya muaji yake.

NI BIASHARA ILIYOIBUKA CHINA?
Ilidaiwa kuwa nchini China imeibuka biashara ya viungo mbalimbali vya binadamu ambapo ili vipatikane ni lazima mwenye viungo hivyo auawe kwa njia yoyote.

SABRINA AFA, MGANDA APOTEA
Mtoa habari wetu alisema wakati Wabongo wakiwa kwenye maombolezo ya kifo cha Mtanzania huyo, mrembo mwingine raia wa Uganda, nchi ambayo imo ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki amepotea katika mazingira ya kutatanisha nchini humo.
Baadhi ya watu wana wasiwasi kuwa kupotea kwa msichana huyo kunahusiana na kushamiri kwa biashara ya viungo vya binadamu.

SABRINA ALIKWENDAJE CHINA?
Mwezi Julai, mwaka jana, Sabrina alikwenda nchini humo akidanganywa na mwanamke mmoja kwamba atapata kazi kwenye saluni ya wanawake lakini baada ya kufika alijikuta akiingizwa kwenye biashara ya ukahaba bila ridhaa yake mpaka alipokutwa na mkasa huo uliopoteza maisha yake.

TAHADHARI KWA WAREMBO WANAOKWENDA CHINA KUFANYA KAZI SALUNI
Imebainika kuwa, kumeibuka wimbi la Wabongo wanaofanya ‘uwakala’ wa kuwachukua wasichana wa Kitanzania kwa kuwadanganya kwamba wanakwenda kufanya kazi za saluni nchini humo.
Mara baada ya kufika, wasichana hao hunyang’anywa paspoti ili washindwe kuondoka nchini humo na kushinikizwa kujiuza (ukahaba) huku waliowapeleka wakipokea fedha kutoka kwa wateja.

KUIKOMBOA PASPOTI
Habari zilisema kuwa mhusika hurejeshewa paspoti yake baada ya malipo yake kwa ‘wakala’ kufikia dola za Marekani 8,000 (kama shilingi milioni 12), ndipo huachiwa ‘huru’ kuendelea na maisha yake.
Wengi wakishaachiwa hushindwa kurejea Bongo na kujikuta wakiendelea kuuza miili katika mahoteli na klabu huku wakikutana na majanga mbalimbali.

MASOGANGE, KAJALA NA DIDA
Watanzania waishio nchini humo wamewatahadharisha mastaa wa Bongo, wakiwemo Mtangazaji wa Radio TimesFM, Khadija Shaibu ‘Dida’, msanii wa filamu Kajala Masanja na Video Queen Agnes Gerald ‘Masogange’ ambao hupenda kwenda nchini humo kwa shughuli zao, kutokubali kuwa karibu na mawakala wa kuchukua wasichana Bongo kwa kuwadanganyia kazi ya saluni kwani wanaweza kujikuta pabaya siku moja.

DIDA
Ijumaa Wikienda lilimsaka Dida siku ya Jumamosi iliyopita na kumuuliza kuhusu kuwepo kwa mawakala hao ambapo alikiri kusikia huku akisema warembo wenyewe wanapaswa kuwa macho na udanganyifu huo.
“Najua wapo Wabongo wanaofanya shughuli hiyo, si China tu hata India, unapelekwa kwa ahadi ya kazi ya saluni, ukifika hamna cha saluni wala nini? Warembo wawe makini jamani, nenda China kama una uwezo wako mwenyewe kufanya ‘shoping’ lakini si kupelekwa,” alisema Dida.

BALOZI WA TANZANIA-CHINA
Juzi, Ijumaa Wikienda lilimtafuta Balozi wa Tanzania nchini China, Luteni Jenerali Mstaafu Abdulrahman Shimbo ili azungumze lolote kuhusu tukio la Sabrina, lakini simu yake ilionekana kutokuwa hewani kwa muda mrefu.

Soma Habari Kamili

UGANDA YAPIGA MARUFUKU VIMINI, VITOPU NA MAVAZI MENGINE YA NUSU UCHI.....ATAKAYE KAIDI, ATAFUNGWA JELA MIAKA 10 MPAKA 15



RAIS Yoweri Museveni amesaini sheria ambayo inaharamisha mavazi yasiyo ya heshima na picha za utupu. 

Pia, wanawake wamepigwa marufuku kuvaa nguo fupi - vimini na blauzi fupi – vitopu, ambavyo vinashawishi hisia za ngono, isipokuwa kama vivazi hivyo vitatumika kwa madhumuni ya kutoa elimu au matibabu au kutumika kwenye michezo na utamaduni.
 
Akizungumza na waandishi wa habari katika Kituo cha Habari jijini  Kampala  juzi, Waziri wa Nchi anayeshughulikia Maadili, Mchungaji Simon Lokodo, alisema Rais alisaini Muswada huo kuwa sheria Februari 6, miezi miwili baada ya kupitishwa na Bunge Desemba mwaka jana.

Waziri alisema kuwa serikali haitaki watu kuvalia nguo zisizo na heshima na kuzua hisia zisizofaa miongoni mwa watu. Watakaopatikana wakivunja sheria na kuvalia visivyo watafungwa hadi miaka 10 na wale watakaopatiokana na hatia ya kuhusisha watoto katika biashara ya ngono watafungwa hadi miaka 15.
Kwa mujibu wa sheria hiyo, sasa itaundwa Kamati ya Taifa ya Kukabiliana na Ukiukwaji wa Maadili ya Nchi, ambayo itakuwa na wajibu wa kubaini, kukusanya na kuharibu vitu vyote vinavyohusiana na pon*grafia (picha au maandishi yenye kutia ashiki).
 
Kamati hiyo, ambayo wajumbe wake watatoka sekta mbalimbali zikiwamo tasnia za habari na burudani, pia itatoa huduma za kurekebisha tabia kwa waathirika wa ponografia.
 
Sheria hiyo dhidi ya ponografia, inatengua na kuchukua nafasi ya Kifungu cha 166 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, na kupanua wigo wa tafsiri ya sheria ya pon*grafia na kuiharamisha.
 
Kwa mujibu wa sheria hiyo, pon*grafia inamaanisha “chochote kitakachotolewa kupitia chapisho, maonesho, filamu, teknolojia ya mawasiliano au kwa njia nyingine yoyote, kinachoonesha mtu akiwa katika tendo halisia au maigizo ya ngono au kuonesha sehemu za siri za mtu kwa ajili ya kusababisha ashiki.”
 
Waziri Lokodo pia alitaja matangazo mafupi ya ngono maarufu kama bimansulo, video au picha za ngono kwa watoto, na wanamuziki, hususan wasanii wa kike, ambao hucheza wakiwa wamevalia nguo fupi, kwamba navyo vimepigwa marufuku.
 
“Hatupendi mwonekane katika hali ambayo inavuta hisia za watu wengine. Kuweni na staha na nguo zenu zikuonesheni kuwa watu wenye staha,” alisema Lokodo.
 
Alipotakiwa kufafanua kuhusu uvaaji usio na staha, Waziri alisema: “Kama utavaa vazi ambalo linatatiza fikra na kushitua watu wengine hususan wa jinsia tofauti, umevaa vibaya na tafadhali harakisha kubadilisha vazi lako.”
 
Vituo vya habari navyo vimepigwa marufuku, kuchapisha picha za watu wawili wakibusiana au wanawake waliovaa vibaya kama wanaoonekana katika klabu za usiku, kwa mujibu wa Patricia Achan-Okiria, Ofisa Mkuu wa Sheria katika Wizara ya Maadili.
 
Waziri huyo alielezea wasiwasi unaooneshwa na wabia wa maendeleo juu ya muswada wa kupinga pon*grafia, kama jambo ambalo halitaweza kuiondoa ofisi yake kwenye mapambano dhidi ya mmomonyoko wa maadili katika jamii.

Soma Habari Kamili

FACEBOOK YASEMA ITAINUNUA WHATSAPP ILI KUONGEZA THAMANI YAKE

 
Kampuni ya mtandao wa Kijamii ya Facebook imesema kuwa itanunua mtandao wa mawasiliano ya ujumbe mfupi wa WhatsApp kwa kima cha dola bilioni 16, na nyongeza zaidi ya dola bilioni 3 zitakazolipwa waanzilishi wa mtandao huo pamoja na wafanyikazi wake.
 
Hiyo ndiyo biashara kubwa zaidi ya ununuzi kuwahi kutekelezwa na Facebook hadi kufikia sasa.
 
WhatsApp ni maarufu sana miongoni mwa vijana wanaotafuta kuepuka kulipia huduma ya kutuma ujumbe mfupi wa simu yaani SMS. WhatsAp imeweza kuwasajili zaidi ya watumiaji milioni 450.
 
Katika taarifa, mwanzilishi wa Facebook Mark Zuckerberg amesema kuwa mtandao huo upo njiani kuwaunganisha watu bilioni moja jambo  ambalo  litaifanya Facebook kuwa na thamani kubwa.

Soma Habari Kamili

WATOTO WAWILI WA KIUME WA KIAFRIKA WATUPWA JELA BAADA YA KUPIGWA MABUSU NA MTOTO WA KIKE WA KIZUNGU



In 1958, two African American boys were playing with friends in the White section of their North Carolina town. It was an innocent time in their lives. James Hanover Thompson was 9 and David Simpson was 7 years old at the time.



While playing, a friend suggested that one of the little white girls they were playing with give the two boys a kiss- and she did. James told NPR.org, “The little girl gave me a peck on the check and then she kissed David on the check. So, we didn’t think nothing of it. We were just little kids.”

What happened next will blow your mind. The little girl went home and casually mentioned the kiss to her parents, who became furious and called the police.

The two young boys were eventually detained and charged with rape and later molestation.

The night they were hauled off to jail, they were badly beaten by police officers; and the officers made sure only to hit the boys upon their bodies. James stated, “They didn’t beat us to the face, where nobody could see it; they just punched us all in the stomach and back and legs. We was hollering and screaming. We thought they was gonna kill us.”

The two boys weren’t allowed to see their mothers for weeks, but their case soon caught the attention of the media and an international committee was formed in Europe to defend the children.

Joyce Egginton a London based journalist, was granted an interview with the boys. She smuggled a camera into the jail and brought their mothers along. There she took pictures of the women hugging their sons and published the story in the London Observer. Soon the story spread throughout Europe and Asia, which embarrassed the United States.

In the interim, the boys were sentenced to reform school until their 21st birthdays.
The boys were eventually pardoned by the Governor after spending three months in detention. They never received an apology.

Their lives and the lives of their families were subsequently ruined. James’s mother was a nervous wreck while her son was locked up. Her daughter Brenda recalls, “She didn’t sleep. She would be up walking the floors and praying.”

Also, the family faced further tοrture as the KKK regularly visited the family’s home and burned crosses on their front lawn. They also occasionally shot at their house. “My mom and them, they would go out in the morning and sweep bullets off our front porch,” Brenda further stated.

James and David have never spoken about what happened to them in the prison - the memories were too painful to bear. But their lives were forever turned upside down with James spending most of his life in and out of prison.
James told NPR.org, “I always sit around and I wonder, if this hadn’t happened to me, you know, what could I have turned out to be? Could I have been a doctor? Could I have went off to some college, or some great school? It just destroyed my life.”

There is no word on the outcome of the youngest victim, David Simpson.



Soma Habari Kamili

HAWA NDIO WANACHAMA WA FREEMASON TANZANIA



Tanzania ina wanachama hai zaidi ya 600 wa kundi la watu wenye imani ya siri ya Freemasons wakiwa wanatokana na watu wa kada mbalimbali wakiwemo maarufu, huku ikielezwa kwamba miongoni mwao hakuna viongozi wakuu wa serikali.

Hayo yalibainishwa na Kiongozi wa kundi la Freemasons katika eneo la Afrika Mashariki, Jayantilal Keshavji Chande maarufu kama Sir Andy Chande.
Kiongozi huyo Mtanzania mkazi wa Dar es Salaam mwenye asili ya Kiasia, alisema licha ya Tanzania kuwa na wanachama hao, kwa sasa idadi ya wanachama duniani inapungua tofauti na inavyoonekana sasa kuwa wanaongezeka kutokana na kuibuka maneno mengi kuhusu kundi hilo.

Alisisitiza kuwa si rahisi kumjua mwanachama wa kundi hilo, bali wenyewe ndio wanaofahamiana, akisema ni siri na kwamba wenyewe wanakutana katika vikao mbalimbali mara moja kwa mwezi au zaidi.

Alisema nchini kuna wanachama zaidi ya 600 wakiwemo wafanyabiashara, watumishi serikalini, walimu pamoja na wanataaluma mbalimbali wanaoheshimika sana na kusisitiza kuwa kuna maneno mengi yanayosemwa kuhusu kundi hilo, ambayo siyo ya kweli.

Alisema idadi ya wanachama wake duniani inazidi kupungua kutoka milioni nane hadi sasa wako milioni sita, tofauti na wengi wanaodhani kuwa idadi hiyo inaongezeka.

Chande alizungumza na mwandishi wa habari hizi katika Shule ya Sekondari ya Shaaban Robert ambako yeye ni Mwenyekiti wa Bodi ya shule alipozungumzia maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwake.


Alisema duniani kuna watu wazito wengi ambao ni wanachama wa kundi hilo kama majaji wakubwa na hata Binamu wa Malkia Elizabeth wa Uingereza ni kiongozi mkubwa wa kundi hilo.

Akizungumzia masharti ya kujiunga na kundi hilo, Chande alisema ni lazima mwanachama huyo awe anaamini katika Mungu bila kubagua iwapo ni Mkristo au Muislamu.


Alisema pia ni lazima anayetaka kujiunga awe na umri unaozidi miaka 21 na walio chini ya umri huo hawaruhusiwi kujiunga na lazima familia ya anayetaka kujiunga na wanandugu wafahamu kuwa umejiunga na kundi hilo.

Soma Habari Kamili

MCHEZA MIELEKA MAARUFU DUNIANI BIG DADDY V AFARIKI DUNIA

Big Daddy V enzi za uhai wake.
Big Daddy V akiwa kazini enzi za uhai wake.
Mwanamieleka wa WWE, Nelson Frazier maarufu kama Mabel, Viscera na Big Daddy V amefariki dunia kwa ugonjwa wa moyo jana Jumanne. Big Daddy V amefariki akiwa na umri wa miaka 43.

Soma Habari Kamili

BALOZI ZISAIDIE KUUTANGAZA UTAMADUNI WETU‏ - SALMA MOSHI


Msanii aliyetamba enzi hizo kwa umahiri wake wa kucheza na nyoka, Salma Moshi akisalimiana na kumkabidhi picha za baadhi ya kazi ya sanaa hiyo aliyofanya enzi hizo Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani, Mhe. Liberata Mulamula alipokwenda kujitambulisha rasmi kwenye Ubalozi wa Tanzania uliopo Washington, DC siku ya Jumanne Feb 18, 2014.
Msanii wa siku nyingi na mahiri wa kucheza na nyoka, Bi. Salma Moshi aliongea na Mhe. Balozi Libetara Mulamula alipotembelea Ubalozi wa Tanzania Washington, DC siku ya Jumanne Feb 18, 2014.
Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tamzania nchini Marekani, Mhe. Liberata Mulamula akimsikiliza msanii wa siku nyingi, Bi. Salma Moshi (hayupo pichani) alipotembelea Ubalozi wa Tanzania Washington, DC siku ya Jumanne Feb 18, 2014.
 Afisa Mgendi Nzowa akiwa kwenye mkutano huo.
 Afisa Suleiman Saleh akijumuika pamoja na Balozi kwenye mkutano huo.
Wito hou umetolewana msanii wa siku nyingi wa kucheza na nyoka Mama Salma Moshi alipokwenda kumuona Mhe. Balozi Liberata Mulamula ambaye ni Balozi wa Tanzania nchini Marekani. Mama Salma alisema Balozi zina nafasi nzuri za kuutangaza utamaduni wetu kwani wapo karibu na nchi husika na hivyo kuviwezesha vikundi kuja kufanya maonyesho pia aliomba BARAZA LA SANAA LA TAIFA kuandaa kitabu kitakachojumuisha wasanii mbalimbali na anwani zao vitabu hivyo vipelekwe kwenye balozi zetu ili watu mbalimbali wanaokuja waweze kuvisoma na hatimaye kuwaalika wasanii wataweza kuutangaza utamaduni wetu na wasanii kujipatia kipato na pia kujifunza. 
Mama Salma alisema MAPROMOTA wengi baada ya kupata wamekuwa wanawatelekeza wasanii na pato kubwa linaenda kwao bili kunufaisha msanii na hata wale wanaobahatika kuja kupiga nje wamekuwa wanaishia kuwapigia Watanzania ifike wakati wakija huku waweze kutumbuiza na wenyeji wa huku alitoa mfano kama Jay Z aende Tanzania halafu awapigie WAMEREKANI. Mama Salma alikemea vikali swala la kukopi kazi za sanaa linarudusha nyuma maendeleo ya wasanii na aliomba SERIKALI kutoa adhabu kali kwa watakaobainika na kusimamia swala la hakimiliki Mama Salma alisema imefika wakati sasa wasanii kuwa na WANASHERIA hii itasaidia kulinda haki zao. Mama Salma alimshukuru sana MHE. RAIS ambaye amekuwa wakati wote karibu na wasanii na hata hivi karibuni aliwaalika kwenye chakula hivyo naomba wasanii tuitumie nafasi hiyo.
Alisema kuhusu tuzo ziwe zinatoka kwa wasanii wa sanaa za maonyesho na wakati umefika kutoa kibali kwa waandaaji wengine si vibaya zikawa zaidi ya moja pia aliomba kusaidia kujenga maktaba kwenye eneo la viwanja vya wasanii MKURANGA na kumpongeza mwenyekiti wa wasanii BWANA TWALIBU.  MH BALOZI alimshukuru sana msanii huyo na kumpongeza kwa kazi nzuri ya kuwakilisha nchi na kuwa msanii atakayekuwa mfano kwa wengine. Aliongeza kuwa kuhusu Hakimiliki SERIKALI imejizatiti kikamilifu kuhakikisha haki za msanii zinalindwa na ni vyema wasanii wakajua haki zao.

Soma Habari Kamili

TAMKO LA RAIS BARACK OBAMA WA MAREKANI JUU YA MSWADA WA KUPINGA USHOGA UGANDA


President Barack Obama.
As a country and a people, the United States has consistently stood for the protection of fundamental freedoms and universal human rights. We believe that people everywhere should be treated equally, with dignity and respect, and that they should have the opportunity to reach their fullest potential, no matter who they are or whom they love.


That is why I am so deeply disappointed that Uganda will shortly enact legislation that would criminalize homosexuality. The Anti-Homosexuality Bill in Uganda, once law, will be more than an affront and a danger to the gay community in Uganda. It will be a step backward for all Ugandans and reflect poorly on Uganda’s commitment to protecting the human rights of its people. It also will mark a serious setback for all those around the world who share a commitment to freedom, justice and equal rights.

As we have conveyed to President Museveni, enacting this legislation will complicate our valued relationship with Uganda. At a time when, tragically, we are seeing an increase in reports of violence and harassment targeting members of the LGBT community from Russia to Nigeria, I salute all those in Uganda and around the world who remain committed to respecting the human rights and fundamental human dignity of all persons.
SOURCE
The White House

Soma Habari Kamili

Ungana Nasi, Like Page Yetu Hapa Chini