KAMPENI ZA CCM JIMBO LA KALENGA ZAZIDI KUPAMBA MOTO


Mgombea kwa tiketi ya CCM katika Uchaguzi Mdogo jimbo la Kalenga, Iringa Vijijini, Godfrey Mgimwa (wapili kushoto), Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu na Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Bara Mwigulu Nchemba, wakiserebuka na wananchi baada ya kuwasili katika Kijiji ya Kibebe Kata ya Ulanda kwa ajili ya mkutano wa kampeni, jana.
Mgombea kwa tiketi ya CCM katika Uchaguzi Mdogo jimbo la Kalenga, Iringa Vijijini, Godfrey Mgimwa (kushoto) akiwasalimia wananchi kwa kuwapungia mkono, baada ya kuwasili katika Kijiji ya Kibebe Kata ya Ulanda kwa ajili ya mkutano wa kampeni. pamoja naye ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wsa Iringa, Jesca Msambatavangu na Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Mwigulu Nchemba.
Wananchi wa Kijiji ya Kibebe Kata ya Ulanda, wakiwa wamembeba kumpeleka kitini mgombea wa CCM jimbo la Kalenga Godfrey Mgimwa, alipowasili kwenye kijiji hicho kufanya mkutano wa hadhara.
Mwenyekiti wa CCM Iringa, Jesca Msambatavangu akihutubia mkutano wa kampeni za uchaguzi mdogo jimbo la kalenga, katika Kijiji ya Kibebe Kata ya Ulanda.
Ni shangwe na nderemo kwa wananchi wa kijiji ya Kibebe ya Ulanda katika mapokezi ya mgombea wa CCM alipowasili eneo lao.
Mwana-CCM Maria Geofrey, akiwa ameketi kivulini na mtoto wake, wakati wa mkutano wa kampeni ulipokuwa kifanyika katika Kijiji ya Kibebe Kata ya Ulanda.
Mama akichota maji safi na salama, Kijiji ya Kibebe Kata ya Ulanda, jimbo la Kalenga, Iringa Vijijini, wakati CCM wakiendelea na mkutano wa kampeni katika eneo hili. Kwa mujibu wa wenyeji kisima hicho cha maji kilichimbwa na Mbunge wa zamani wa jimbo la Kalenga, Marehemu Dk. William Mgimwa, ambaye alifariji Januari Mosi, mwaka huu, na kusababisha jimbo kuingia katika uchaguzi mdogo. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

Post a Comment

Ungana Nasi, Like Page Yetu Hapa Chini