MLELA ATUPIWA DONGO KUWA TEJA

Nyota wa filamu za Kibongo, Yusuph Mlela
NYOTA wa filamu za Kibongo, Yusuph Mlela amedaiwa kugeuka teja (mbwia madawa ya kulevya) hali inayomsababishia ashindwe kujichanganya na wasanii wenzake katika shughuli mbalimbali.
Kikizungumza na Amani juzikati, chanzo  kilisema msanii huyo kwa sasa anavuta unga kiasi cha uteja kujionesha waziwazi na kupoteza mwonekano wake wa zamani.
Juzi, paparazi wetu alimtafuta Mlela na kufanikiwa kumpata nyumbani kwao Kinondoni jijini Dar es Salaam ambapo alikuwa na haya ya kusema:
“Katika maisha yangu sijawahi kutumia madawa ya kulevya na huwa nayapinga sana. Wanaosema navuta ni waongo, mimi sasa hivi naitwa baba, hivyo majukumu yameongezeka ndiyo maana sijichanganyi kivile.”

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

Post a Comment

Ungana Nasi, Like Page Yetu Hapa Chini