STEVE NYERERE: LULU NI BINTI MDOGO ILA ANAJITAMBUA TOFAUTI NA WASANII WENGINE WAKUBWA


Elizabeth Michael ‘Lulu’.
RAIS wa Bongo Movie Unit, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ amemmwagia sifa staa wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ kuwa ni binti mdogo lakini sasa anajitambua tofauti na wasanii wengine wakubwa.
Akipiga stori na Ijumaa Steve alisema kuwa, mbali na umakini katika kazi zake za kisanii, sasa hivi yuko makini sana na maisha yake kiasi kwamba ni nadra sana kumkuta na skendo za kijingajinga.
Steve Nyerere.
“Achilia mbali hao mastaa wote unaowajua wewe, mimi nikiwa kama kiongozi wa Bongo Movie siwezi kusema uongo, namkubali sana Lulu kwani ni binti mdogo na anajitambua na sasa siyo mtu wa kuendekeza mambo ya starehe kama wengine, pia huwezi kumuona viwanja kirahisi, katulia anafanya kazi,” alisema rais huyo.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

Post a Comment

Ungana Nasi, Like Page Yetu Hapa Chini