PICHA ZA MILIPUKO YA MABOMU ILIYOTOKEA ZANZIBAR LEO MCHANA

 
Eneo ambalo limeharibika kwa kuchimbika na kitu cha mlipuko katika eneo la mkunazini, na kuleta mtafaruku  katika majira ya mchana..Katika mlipuko huo hakuna mtu aliyepata majeraha na uharibifu wa majengo katika eneo hilo.   
 Mkuu wa Wilaya ya Mjini Unguja Mhe Abdi Mahmoud Mzee akizungumza na Kiongozi wa Kanisa la Mkunazini Ndg. Nuhu Salanya, na Maofsa wa JWTZ , katika eneo la tukio na kutoa maelekezo kwa Uongozi wa Kanisa alipofika katika eneo la tukio kuangalia athari na uharibifu uliotokea katika eneo hilo wakati wa mlipuko huo. 
Mkuu wa Wilaya ya Mjini Mhe Abdi Mahmoud Mzee akizungumza na Makamanda wa JWTZ waliofika eneo la tukio kuagalia na kuchunguza tukio hilo la mlipuko katika eneo la Mkunazini
Maofisa wa JWTZ wakiangalia eneo la tukio lililochimbika kutokana na kitu kinachodhaniwa ni bomu, katika tukio hilo hakuna Mwananchi aliyejeruhiwa.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

Post a Comment

Ungana Nasi, Like Page Yetu Hapa Chini