Halimashauri ya jiji la Arusha imebomoa nyumba zaidi ya 330
baada ya kushinda kesi iliyofunguliwa na waliokuwa wapangaji
waliokuwa wakipinga amri ya kuhama kupisha zoezi la ujenzi wa
nyumba za kisasa.
Mradi wa ujenzi wa nyumba za kisasa unatekelezwa na Halmashauri ya jiji kwa kushirikiana na wadau mbali mbali.
Bomoa bomoa hiyo ilianza jana alfajiri na wananchi wakiwemo vijana walitoa ushirikiano wa kufanikisha zoezi hilo huku baadhi ya wapangaji wakiwalaumu wanasiasa kwa kuwapotezea muda na gharama kubwa ya kwenda mahakamani wakijua wazi kuwa hawatashinda kesi hiyo.
Abdalah Hassan Mmbaga na zainabu jabiri ambao ni miongoni mwa wananchi ambao nyumba zao zilibomolewa, walisema inashangaza kuona wakati wa zoezi hilo wanasiasa wanajiweka pembeni wakati wao ndio waliokuwa vinara wa kuwapa wananchi moyo kuwa watawasaidia na hawatahamishwa.
“Kwenye uchaguzi mdogo wa madiwani wa Kata nne, tukiwa eneo la Ilboru Naibu Meya wa Jiji la Arusha alituhakikishia kwamba notisi zimesimamishwa hivyo wapangaji tusubirie mpaka tamko litakapotoka.
Mwanasheria wa jiji la Arusha, Kiomoni Kiburwa na Mkuu wa wilaya, John Mongela wamesema zoezi la ubomoaji limezingatia taratibu zote za kisheria na haki za pande zote zikiwemo za wapangaji ambao walipewa muda wa kutosha wa kuhamisha vitu vyao.
Kibamba alisema uamuzi huo umekuja baada ya kuwapo kwa majibizano ya muda mrefu baina ya wapangaji wao 216 na Halmashauri hiyo waliokuwa wakiongozwa na Sumari.
Alisema kwa miaka mingi Halmashauri hiyo ilipanga kuyaendeleza maeneo hayo kwa kuvunja nyumba za zamani na kukaribisha uwekezaji mkubwa lakini waliokuwa wapangaji wao waligoma na kukimbilia mahakamani.
Kiomoni alisema kabla ya kukimbilia mahakamani kufungua kesi wapangaji wao waliweka masharti magumu matatu dhidi ya mwenye nyumba wakitaka kupewa fidia ya kukaa kwenye nyumba hizo.
Alisema masharti mengine yalikuwa ni Halmashauri iwajibike kuwatafutia viwanja kwingine ili wakajenge na la mwisho kuwa waangaji hao walitaka kupangishwa kwenye uwekezaji utakaofanywa,” alisema Kiomoni.
“Tumewahi kuiomba Mahakama iwape notisi ya miezi sita kuanzia Januari 11, Mwaka 2013 wakae bila malipo wakati wakitafuta nyumba kwingine. Juni 10, Mwaka 2013 ilikuwa ukomo wa notisi iliyotolewa hivyo Jiji lilitaka kuvunja nyumba zake.
“Wapangaji walikwenda Mahakama Kuu wakafungua kesi namba 23 ya 2013 hivyo ilitolewa amri ya zuio la muda hadi hapo madai yao yatakaposikilizwa. Lakini na sisi tuliweka pingamizi kwamba hapakuwa na mgogoro kati yetu na wapangaji.
Hata hivyo kuvunjwa kwa nyumba hizo kumeleta neema kwa baadhi ya watu wakiwamo vijana wanaokusanya vyuma chakavu kuvamia maeneo hayo na kuokota kila aina ya chumba au kitu ambacho waliamini kinaweza kuuzwa na kuwapatia fedha.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo amewataka wakazi wa arusha wakiwamo wanaohamishwa kutambua kuwa zoezi hilo linafanyika kwa nia njema ya kuboresha jiji kwa maslahi wananchi wote na taifa na kuomba kuendelea kutoa ushirikiano wa kukabiliana na changamoto mbali mbali zinazokwamisha maendeleo .
Mradi wa ujenzi wa nyumba za kisasa unatekelezwa na Halmashauri ya jiji kwa kushirikiana na wadau mbali mbali.
Bomoa bomoa hiyo ilianza jana alfajiri na wananchi wakiwemo vijana walitoa ushirikiano wa kufanikisha zoezi hilo huku baadhi ya wapangaji wakiwalaumu wanasiasa kwa kuwapotezea muda na gharama kubwa ya kwenda mahakamani wakijua wazi kuwa hawatashinda kesi hiyo.
Abdalah Hassan Mmbaga na zainabu jabiri ambao ni miongoni mwa wananchi ambao nyumba zao zilibomolewa, walisema inashangaza kuona wakati wa zoezi hilo wanasiasa wanajiweka pembeni wakati wao ndio waliokuwa vinara wa kuwapa wananchi moyo kuwa watawasaidia na hawatahamishwa.
“Kwenye uchaguzi mdogo wa madiwani wa Kata nne, tukiwa eneo la Ilboru Naibu Meya wa Jiji la Arusha alituhakikishia kwamba notisi zimesimamishwa hivyo wapangaji tusubirie mpaka tamko litakapotoka.
Mwanasheria wa jiji la Arusha, Kiomoni Kiburwa na Mkuu wa wilaya, John Mongela wamesema zoezi la ubomoaji limezingatia taratibu zote za kisheria na haki za pande zote zikiwemo za wapangaji ambao walipewa muda wa kutosha wa kuhamisha vitu vyao.
Kibamba alisema uamuzi huo umekuja baada ya kuwapo kwa majibizano ya muda mrefu baina ya wapangaji wao 216 na Halmashauri hiyo waliokuwa wakiongozwa na Sumari.
Alisema kwa miaka mingi Halmashauri hiyo ilipanga kuyaendeleza maeneo hayo kwa kuvunja nyumba za zamani na kukaribisha uwekezaji mkubwa lakini waliokuwa wapangaji wao waligoma na kukimbilia mahakamani.
Kiomoni alisema kabla ya kukimbilia mahakamani kufungua kesi wapangaji wao waliweka masharti magumu matatu dhidi ya mwenye nyumba wakitaka kupewa fidia ya kukaa kwenye nyumba hizo.
Alisema masharti mengine yalikuwa ni Halmashauri iwajibike kuwatafutia viwanja kwingine ili wakajenge na la mwisho kuwa waangaji hao walitaka kupangishwa kwenye uwekezaji utakaofanywa,” alisema Kiomoni.
“Tumewahi kuiomba Mahakama iwape notisi ya miezi sita kuanzia Januari 11, Mwaka 2013 wakae bila malipo wakati wakitafuta nyumba kwingine. Juni 10, Mwaka 2013 ilikuwa ukomo wa notisi iliyotolewa hivyo Jiji lilitaka kuvunja nyumba zake.
“Wapangaji walikwenda Mahakama Kuu wakafungua kesi namba 23 ya 2013 hivyo ilitolewa amri ya zuio la muda hadi hapo madai yao yatakaposikilizwa. Lakini na sisi tuliweka pingamizi kwamba hapakuwa na mgogoro kati yetu na wapangaji.
Hata hivyo kuvunjwa kwa nyumba hizo kumeleta neema kwa baadhi ya watu wakiwamo vijana wanaokusanya vyuma chakavu kuvamia maeneo hayo na kuokota kila aina ya chumba au kitu ambacho waliamini kinaweza kuuzwa na kuwapatia fedha.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo amewataka wakazi wa arusha wakiwamo wanaohamishwa kutambua kuwa zoezi hilo linafanyika kwa nia njema ya kuboresha jiji kwa maslahi wananchi wote na taifa na kuomba kuendelea kutoa ushirikiano wa kukabiliana na changamoto mbali mbali zinazokwamisha maendeleo .
0 comments:
Post a Comment