MIAKA 20 YA NDOA, DEVOTA AZAWADIWA GARI

Devota Mbaga
Katibu Msaidizi wa Bongo Movie Unity, Devota Mbaga amezawadiwa gari aina ya Toyota Harrier Lexus na mumewe aliyemtaja kwa jina la Mr. Mbaga baada ya kudumu katika ndoa kwa muda wa miaka 20.
 
Akizungumza na Ijumaa, Devota alisema anamshukuru Mungu kwa kukaa katika ndoa yake kwa amani na hatimaye kutimiza miaka hiyo kwani ni wachache wanaotimiza umri huo.
Devota akipozi na gari lake alilozawadiwa.
“Siku niliyotimiza miaka hiyo nilikuwa nimejisahau lakini mume wangu alithamini na kunishtukiza kwa kunizawadia gari ambalo aliliandika jina langu kwenye kioo cha ‘sight mirror’ upande wa kushoto, namshukuru Mungu na mume wangu pia,” alisema Devota.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

Post a Comment

Ungana Nasi, Like Page Yetu Hapa Chini