BABA KANUMBA: NITAMPELEKA MAMA KANUMBA SEGEREA



 http://api.ning.com/files/BrAPCEwtvYDNlrlYwAb0FlxzgXMaaorbIDZlHTjKWPHV0Xvq1g*W6OqvzSs2cy2sJ7XYhr8r1y1mE5svyJwDilEhD38B*TMe/BabaKanumba2.jpg?width=640
BABA wa marehemu Steven Kanumba, Charles Kanumba anaonekana kuendelea kuwewesekea mali za mwanaye baada ya kuibuka na kudai kuwa, atampeleka Segerea (jela) mzazi mwenzake, Flora Mtegoa kwa madai kuwa amezifuja mali za marehemu.
Mama Kanumba, Flora Mtegoa.
Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni kwa njia ya simu, baba Kanumba alisema, ameona taarifa kwenye gazeti kuwa mali nyingi za marehemu Kanumba zimeuzwa huku yeye akiwa hajaambulia chochote.
“Huyu mama Kanumba ana laana yangu, amefuja mali za mwanangu kwa kushirikiana na Seth, mimi sijashirikishwa, nisipopata chochote tutafikishana pabaya,” alisema mzee huyo.
Baba wa marehemu Kanumba, Charles Kanumba.
Kuhusiana na hilo, mama Kanumba huyu hapa: “Kwa mila za Kisukuma Kanumba siyo mwanaye kwa kuwa hajanioa, hivyo kuhusu suala la mali kama anazijua zinazomhusu aonyeshe moja baada ya nyingine hapo itakuwa sawa.”

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

Post a Comment

Ungana Nasi, Like Page Yetu Hapa Chini