Halima Yahya ‘Davina’, staa wa sinema Bongo, amefunguka kuwa
anajitahidi kufanya mazoezi ili mwili wake usizeeke akaachika kwa
mumewe. Akipiga stori na paparazi wetu, Davina alisema mikakati yake ni kuhakikisha ndoa yake inashamiri miaka yote. “Sikubali kuachika, siri ya kulinda ndoa yangu ni mazoezi tu, acha nijifue mwanzo mwisho,” alitamba Davina.
0 comments:
Post a Comment