KILICHOWAPONZA MAWAZIRI WA KIKWETE CHABAINIKIA, KISIPOREKEBISHWA, MAWAZIRI WENGI WATAENDELEA KUNG'OLEWA



MKUU wa Wilaya ya Bunda, Joshua Mirumbe, amekerwa na tabia ya watendaji wengi wa serikali kutowajibika ipasavyo na matokeo yake kuwabebesha mizigo mawaziri na Rais.
 
Alisema chanzo cha wizara nyingi kutofanya vizuri kunasababishwa na mfumo mbaya ulioendekezwa na baadhi ya wakurugenzi,makamishna, makatibu na watendaji walioko chini yao kukosa uzalendo wa kuwajibika kwa wananchi.
 
Akitoa hutuba fupi jana katika mkutano mkuu wa mwaka wa Chama cha Akiba na Mikopo cha Bunda (Bunda SACCOS), alisema wananchi wako tayari kuwajibika isipokuwa kikwazo ni baaadhi ya watendaji hao wa serikali kuwa miungu watu.
 
Aliongeza kuwa sheria ya utumishi ya kuwachukulia hatua za kisheria watendaji wasiowajibika ina mlolongo mrefu jambo linalokwamisha uwajibikaji, hivyo alishauri sheria hizo zirekebishwe.
 
Mirumbe alisema shughuli nyingi za Serikali hukwamishwa na watumishi wa kati ngazi za halmashauri, mikoa na kwenye wizara huku wakijua kuwa mishahara yao ni kodi ya wananchi wanaonyanyaswa.
 
Alikuwa akijibu taarifa ya Mwenyekiti wa SACCOS hiyo, John Kitang’osa, aliyesema kuwa yapo maombi mengi ambayo wamepeleka kwa Serikali kupitia taasisi zake, lakini majibu hayatolewi kwa wakati muafaka.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

Post a Comment

Ungana Nasi, Like Page Yetu Hapa Chini