MAINDA AACHANA NA UIGIZAJI WA FILAMU ZA KIBONGO, AMRUDIA MUNGU NA KUANZA KUIMBA NYIMBO ZA INJILI!

Msanii wa sinema Bongo, Ruth Suka ‘Mainda’
MSANII wa sinema Bongo, Ruth Suka ‘Mainda’  aliyewahi kutamba na filamu za kidunia, sasa ameamua kuimba muziki wa Injili ikiwa ni kumtukuza Mungu na kujiandalia maisha mema ya peponi.
Akipiga stori na mwandishi wetu juzi, staa huyo aliyekuwa akiitwa Mwanaidi na kubadili jina baada ya kuokoka, alisema: Vijana siku zote tuna nguvu, tuna muda wa kutosha hivyo tunapaswa kumtumikia Mungu siyo mpaka tuchoke, tuzeeke au tufanye kwanza dhambi ikifika omega (mwisho) ndiyo unamkumbuka Mungu.
Mainda akiwa kwenye pozi
“Ninaimba kwaya tena sauti ya tatu, subirini muone ujio wangu mpya kwani nimeamua kumtukuza Mungu aliyeumba mbingu na nchi.”

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

Post a Comment

Ungana Nasi, Like Page Yetu Hapa Chini