WAJUMBE wa Bunge Maalum la Katiba wameshauriwa kutokuwa watumwa wa kupokea maagizo ya vyama vyao vya siasa kwa hofu ya kupoteza madaraka, kwani wakifanya hivyo watakuwa hawatendei haki wananchi.
Kauli
hiyo ilitolewa jana na mfanyabiashara wa mjini Dodoma, Augustino
Ndejembi alipokuwa akielezea jinsi mchakato mzima wa Bunge la Katiba
unavyoendelea.
Alisema
ikiwa wajumbe wa Bunge hilo wataamua kuingiza mapendekezo ya viongozi
kutakuwa ni ndoto kupatikana kwa katiba itakayogusa maisha ya
Watanzania.
“Ni
muhimu wabunge kukataa kuwa watumwa wa kupokea mapendekezo kutoka kwa
viongozi hao bali tunachotaka kila mmoja awakilishe mawazo yake mwenyewe
hapo tunakuwa tumeipata katiba inayohitajika kwa hivi sasa,”alisema
Ndejembi.
Ndejembi
alisema kuwepo kwa wabunge hao bungeni kunatokana na matakwa ya
wananchi na siyo kwa kuagizwa na viongozi wa siasa ambao wanataka
waingize itikadi za vyama vyao.
Kwa
upande wake, Askofu Mkuu wa Kanisa la Gospel Catholic Tanzania, Daud
Chidawali aliwataka wajumbe hao, kutonunuliwa na viongozi wa siasa na
dini ili wapitishiwe miswada wanayopenda wao.
Alisema
kwa kufanya hivyo nchi inaweza kuingia pabaya na kusababisha hata
migogoro, inayoweza kuzaa vita kama nchi za jirani zilivyo kwa hivi
sasa.
Chidawali
alisema Watanzania wanahitaji kuipata katiba isiyofungamana na upande
wowote ule, ambao utaonekana kama katiba hiyo ni ya kwao.
Katibu
Mkuu wa Kituo cha Kiislamu cha Dalai, Rashid Bura alisema wajumbe wa
Bunge la Katiba, wakae wakijua wanayo dhima mbele ya Mwenyezi Mungu kwa
kazi waliyotumwa na wananchi na si vyama vyao.
Alisema
wajumbe wameanza kujadili jambo la Muungano zaidi na serikali tatu,
badala ya kujadili mambo ya msingi ambayo ni mengi ikiwemo, kufikiri
wasomi watakwenda wapi wanapokosa ajira ili isije ikaleta machafuko
katika nchi, maana palipo na wasomi wengi na hakuna ajira machafuko
huwepo.
Alitaja
mambo mengine muhimu yanayotakiwa kujadiliwa ni haki za msingi za
wananchi, kama kupata haki katika Mahakama, Polisi na sehemu mbalimbali
ambapo haki inatakiwa kutendeka.
“Pia
kuna haki za msingi za wastaafu baada ya kumaliza utumishi wao
wanatakiwa kuishi vipi tumeona mpaka sasa baadhi ya wastaafu hawajapata
haki zao kwa miaka zaidi ya 20 hayo ni masuala ya msingi ya kujadili
katika Katiba na si malumbano kama ilivyo sasa,” alisema.
>>Habari leo
>>Habari leo
0 comments:
Post a Comment