MHE.SAMIA SULUHU HASSAN AMECHAGULIWA KUWA MAKAMU MWENYEKITI WA BUNGE MAALUMU LA KATIBA


Hatimaye leo Bunge maalum la Katiba limemchagua Mhe.Samia Suluhu Hassan kuwa Makamu Mwenyekiti wake mjini Dodoma. 
 
 Hii inakuja baada ya jana kumchagua Mhe.Samweli Sitta kuwa Mwenyekiti. Mhe Hassan alichaguliwa kwa kura 390 sawa na asilimia 74.6 na kumshinda mpinzani wake Amina Abdalla Amour. Kura 7 ziliharibika - kama jana. 
 
 Katibu wa Bunge hilo Maalum ataapishwa na Rais Jakaya Kikwete kesho asubuhi Ikulu ndogo Dodoma. 
 
 Katibu wa Bunge ndiye atakayemwapisha Mwenyekiti na Makamu wake, na Mwenyekiti atawaapisha wajumbe wote, ndipo shughuli itapoanza rasmi ya kuandika katiba mpya. 

Mhe.Samia Suluhu  Hassan (anaye angalia kamera)akipongezwa na aliyekuwa mshindani wake Mhe Amina Abdalla Amour  mara baada ya kutangazwa kuwa mshindi.

Mhe. Samia Suluhu Hassan, Makamu Mwenyekiti wa Bunge 
la Maalum la Katiba mteule Dodoma, akishukuru wajumbe kwa kumchagua  

Wajumbe kinamama wakishangilia mara baada ya Bunge Maalum la Katiba kumpata Makamu Mwenyekiti Mhe.Samia Suluhu Hassan mjini Dodoma leo

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

Post a Comment

Ungana Nasi, Like Page Yetu Hapa Chini