Kama ilivyokuwa imetarajiwa na wengi, mwigizaji
mashuhuri kutoka Kenya Lupita Nyong'o amenyakuwa tuzo ya Oscar ya
mwigizaji msaidizi wa kike kwa jukumu lake la kuelezea masaibu ya Patseh
katika filamu ya utumwa ya ''12 Years A Slave.''



Nyong’o, 31, aliyeshinda tuzo ya Oscar kwenye filamu yake hiyo ya kwanza alipata shangwe za nguvu baada ya kutajwa kuwa mshindi.
Amemshinda muigizaji mwenzie Jennifer Lawrence wa American Hustle” aliyekuwa akitajwa zaidi kuichukua tuzo hiyo. “Yes!” muigizaji huyo alisikika akisema wakati akipokea tuzo hiyo huku akimkumbatia kaka yake, muongozaji wa 12 Years a Slave, Steve McQueen na waigizaji wengine wa filamu hiyo.



Nyong’o, 31, aliyeshinda tuzo ya Oscar kwenye filamu yake hiyo ya kwanza alipata shangwe za nguvu baada ya kutajwa kuwa mshindi.
Amemshinda muigizaji mwenzie Jennifer Lawrence wa American Hustle” aliyekuwa akitajwa zaidi kuichukua tuzo hiyo. “Yes!” muigizaji huyo alisikika akisema wakati akipokea tuzo hiyo huku akimkumbatia kaka yake, muongozaji wa 12 Years a Slave, Steve McQueen na waigizaji wengine wa filamu hiyo.
Baada ya kupokea
tuzo hiyo Lupita amesema " Haikwepi mawazo yangu kwamba hata dakika
moja ya furaha katika maisha yangu ni shukran na maumivu makubwa kwa mtu
mwingine.''
Kisha Lupita akaongeza kusema, " Na iwe ukumbusho kwangu na kila mtoto kwamba kokote unakotoka, ndoto zako ni halisi.''
Sherehe ya kutolewa kwa tuzo hizo zimefanyika mjini Los Angeles nchini Marekani.
0 comments:
Post a Comment