FLORA MVUNGI ALIZWA NA VIBAKA

STAA wa sinema za Kibongo, Flora Mvungi  ameeleza masikitiko yake baada ya kuibiwa na vibaka.
Kioo kilichovunjwa pamoja na sehemu zilizoibiwa vitu kwenye gari hilo.
Akizungumza na paparazi wetu, Flora alisema siku ya tukio mumewe H. Baba alitoka na gari lake aina ya Toyota I.S.T kwenda mtaa wa Lumumba-Kariakoo, akapaki na kuingia kwenye mizunguko yake lakini aliporejea alishtuka baada ya kukuta kioo kimevunjwa na vitu vilivyokuwemo ndani kuibiwa.
Staa wa sinema za Kibongo, Flora Mvungi
“Vibaka hawana maana wameiba laptop na vitu kibao vidogovidogo ikiwemo flash iliyokuwa na nyimbo tano za mume wangu na wimbo mmojawapo umeshavuja unaitwa Tubebane aliomshirikisha Mellon, inauma sana,” alisema Flora.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

Post a Comment

Ungana Nasi, Like Page Yetu Hapa Chini