BATULI AWAJIA JUU MASTAA WENZAKE WANAOWASHUSHIA HESHIMA KWENYE JAMII


MSANII wa filamu za Kibongo, Yobnesh Yusuph  ‘Batuli’ amesema tabia mbaya za baadhi ya wasanii wenzao ndizo zinazowaharibia na kuwafanya wote waonekane hawana maadili.

Akiongea  na GPL, Batuli alisema amekuwa akipata malalamiko kuwa hawatumii katika filamu zake watoto Jenifer na Jamila waliokuwa wakifanya kazi na marehemu Steven Kanumba, jambo ambalo amelikanusha.
 
“Siwezi kuwanyima watoto nafasi ya kuonyesha vipaji vyao, sema watu hawajui kilichopo nyuma ya pazia. Nimeshawahi kuwaita lakini wazazi wao wakawazuia. Ilibidi nimchukue yule mtoto mwingine mvulana Patrick.
 
“Fikiri nafasi ya msichana inalazimishwa hadi anacheza mvulana ni tatizo. Wasichokijua watu ni kwamba, wazazi wao wanawazuia wakiogopa wataharibika. Wasanii tubadilikeni jamani,” alisema Batuli.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

Post a Comment

Ungana Nasi, Like Page Yetu Hapa Chini