RAY NA MPENZI WAKE CHUCHU HANS WAMMWAGIA CHOKY PESA ZA KUTOSHA


Chuchu Hans na Vincent Kigosi ‘Ray’ katika pozi.
WAPENDANAO, Chuchu Hans na Vincent Kigosi ‘Ray’ waligeuka mapedeshee kwa muda baada ya kummwagia fedha za kutosha, Mkuruguenzi wa Bendi ya Extra Bongo, Ally Choky.
Tukio hilo lililoteka hisia za mashabiki wa bendi hiyo lilitokea juzikati katika Ukumbi wa Meeda, Dar ambapo Ray aliyekuwa ameambatana na ubavu wake huo, walionekana ukumbini humo wakipata vinywaji, baadaye muda ulivyozidi kwenda, wakanogewa na rhumba la Choky na kuanza kutunza. “Mh! Leo mtu na mtuwe wamegeuka mapedeshee, wanamwaga minoti ya kufa mtu, hata hazihesabiki…hatari,” alisikika shabiki mmoja aliyeshuhudia tukio hilo.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

Post a Comment

Ungana Nasi, Like Page Yetu Hapa Chini