MSANII WA BONGO FLEVA 'D MANYUTI' APAGA KUWAFUNIKA P-SQUARE SIKU ZA USONI..!!

 
Mwanamuziki Chipukizi kwenye muziki wa kizazi kipya nchini Abdallah Ramadhani  Manyuti "D-Manyuti" anaetamba na wimbo wake mpya wa "Tamtam" amesema fikra zake kwa sasa ni za kimataifa na si Tanzania tena kwa vile amejipanga kufika huko hivyo kwa uwezo wa Mungu atafika bila shaka. Akiongea na Xdeejayz mwanamuziki huyo alisema" Unajua maisha ni malengo hivyo kila utakachokipanga kitakuwa hivyo kwa hiyo mimi nimepanga kuufikisha muziki wangu kwenye levo ya dunia na naamini Mungu atanijalia hivyo" Alisema mwanamuziki huyo
 
Aidha D-Manyuti anashukuru kwa sasa amepata meneja wa kumsimamia kazi zake ambae anaitwa Maneno ambae nia ndiye meneja burudani Club Jakalanda hivyo anaamini kwa uzoefu mkubwa aliokuwa nao Maneno basi atamsaidia kufanikisha ndoto zake .
 Wimbo huo amemshirikisha mwanadada Missyuna na umekuwa wimbo unaoongzwa kupigwa sana kwenye vituo vya redio nchini.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Ungana Nasi, Like Page Yetu Hapa Chini