DROO YA PILI SHINDA MAHELA NA CHAMPIONI NI DESEMBA 23


Na Mwandishi Wetu DROO ya pili ya Shinda Mahela na Championi inatarajiwa kufanyika Desemba 23, mwaka huu kwa ajili ya kuwapa zawadi za Krisimasi washindi wake.

Dereva bajaj akijaza kuponi ya Promosheni ya Shinda Mahela na Championi.
Zawadi ambazo zitatolewa siku hiyo ni runinga bapa ‘flat screen’ itakayoambatana na dekoda yake, dinner set pamoja na jezi za michezo.
Akizungumza na Championi Jumatano, Meneja wa Global Publishers ambao ni wachapishaji wa gazeti hili, Abdallah Mrisho ‘Abby Cool’, alisema wameona ni vyema wakatoa zawadi hizo siku chache kabla ya kusherehekea sikukuu ya Krismasi ili washindi wajiachie na zawadi hizo majumbani kwao huku wakiburudika na sherehe hiyo.
Baadhi ya wasomaji wa Championi wakijipatia zawadi za sabuni kutoka kwa muuza magazeti hayo leo eneo la Mwembeyanga, Temeke jijini Dar.
Alisema bado kuponi zinaendelea kupokewa ambapo wasomaji wameonekana kuzitaka zawadi hizo ili kuongeza furaha kwenye sikukuu hiyo kubwa.
“Wasomaji hatutakiwi kuwaacha hivihivi kwenye sikukuu ya Krismasi kwani tumeamua kutoa zawadi mapema sana ili ikifika siku hiyo waburudike na familia zao wakiwa na ukumbusho kutoka Championi.
...Mmoja wa wasomaji wa Championi akiwa na nakala yake ya gazeti hilo.
“Wasomaji waendelee tu kuleta kuponi zao, bado tunazipokea, cha muhimu wawahi mapema kabla ya tarehe hiyo ya kuchezeshwa droo,” alisema Mrisho.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Ungana Nasi, Like Page Yetu Hapa Chini