SHIJA ATAMANI KUFUNGA NDOA NA WASTARA

Msanii wa filamu Bongo, Deogratius Shija.
MSANII wa filamu Bongo, Deogratius Shija amefunguka kuwa anatamani sana kumuoa msanii mwenzake, Wastara Juma lakini anaamini kikwazo kitakuwa ni dini.
Akistorisha na paparazzi wetu, Shija alisema tangu kabla msanii huyo hajaolewa na aliyekuwa mumewe, Marehemu Juma Kilowoko ‘Sajuki’, alikuwa anampenda lakini bahati haikuwa yake hivyo kwa sasa anatamani ndoa na mwanamke huyo.
  Msanii wa filamu Bongo, Wastara Juma.
“Unajua natamani sana kumuoa Wastara ila sidhani kama atakubali kubadili dini kwani ni Muislamu haswa, kwa upande wangu siwezi kubadili dini kwa sababu nampenda sana Yesu. Ila ni jambo linalozungumzika,” alisema Shija.
Ijumaa lilifanya jitihada za kumtafuta Wastara ili kuzungumzia ndoto hiyo ya Shija lakini hakuweza kupatikana mara moja.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

Post a Comment

Ungana Nasi, Like Page Yetu Hapa Chini