MGANGA hajigangi! Licha ya kuwa msanii mahiri
anayeelimisha jamii jinsi ya kugundua utapeli na kuepukana nao, Kulwa
Kikumba ‘Dude’ ameibiwa ‘kupigwa’ vifaa vya saluni na vibaka.
Akistorisha na mwanahabari wetu, Dude alisema juzikati vibaka hao
walipanda kwenye dari na kukata ‘celling board’ kisha kuingia ndani ya
saluni yake hiyo ya kike inayosimamiwa na mkewe, maeneo ya Jeti-Lumo,
Dar na kukomba vifaa mbalimbali vyenye thamani ya shilingi milioni tatu
na laki saba.
“Ukweli nimechoka sasa kila siku wananirudisha nyuma kimaendeleo kwa
kuniibia sijui nifanyeje maana imeshakuwa hatari kwangu, wamechukua TV,
madela, redio aina ya sabuufa na vingine vidogovidogo,” alisema Dude
ambaye mwaka 2012 na 2013 aliwahi kulizwa vifaa mbalimbali vya nyumbani.
0 comments:
Post a Comment