MAHAKAMA ya Wilaya ya Geita imemhukumu Selemani Nkwenda (36) kwenda jela mwaka mmoja baada ya kumtia hatiani kwa kutapeli watu kwa kutumia jina la Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye.
Akisoma hukumu hiyo jana, Hakimu wa mahakama hiyo, Zablon Kesase,
alisema ameridhika pasipo shaka kwamba mtuhumiwa alitenda kosa hilo.
Alisema mtuhumiwa huyo alikutwa na makosa mawili na kila kosa
atatumikia kifungo cha miezi sita, hivyo atatumikia kifungo cha mwaka
mmoja jela.
>>Tanzania daima
>>Tanzania daima
0 comments:
Post a Comment