Bwa.Marco Hingi akifurahia mara baada ya kujishindia gari hilo aina ya Noah kutoka kampuni ya Be Forward
****
Kampuni
ya uagizaji wa magari yaliyotumika kutoka JAPAN ya BEFORWARD imeendesha
shindano la kuwapata washindi 25 duniani kote waliojielezea jinsi
wanavyoweza kuitumia kampuni hiyo katika shughuli za maendeleo kupitia
ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa facebook ambapo mtanzania MARCO
HINGI ameibuka mshindi na kujishindia gari.
Akizungumza
jijini DSM Afisa masoko wa kampuni hiyo KOHEI SHIBATA amesema shindano
hilo liliendeshwa wakati wa sikukuu ya CHRISMASS ambapo wateja
waliotembelea ukurasa wa facebook wa befoward walipata nafasi ya
kuulizwa maswali na kujibu mambo kadha wa kadha
Kati
ya washindi hao Tanzania imepata nafasi mbili ambapo mwanafunzi wa chuo
cha afya cha BUGANDO MWANZA bwana MARCO HINGI ameibuka mshindi
Makabidhiano
ya zawadi ya gari aina ya NOAH yenye thamani ya shilingi milioni 11.8
yamefanyika leo jijini DSM kati ya Afisa masoko wa kampuni hiyo KOHEI
SHIBATA na Mshindi MARCO HINGI ambapo SHIBATA amesema hiyo ni moja ya
mikakati yao ya kuongeza mauzo kwa kuwafanya wateja kuwa na imani nao
kama anavyoeleza meneja mkuu ISAAC MBINILE
Kwa
upande wake MARCO HINGI ambaye ni mwanafunzi wa chuo cha afya BUGANDO
mwanza amesema aliwaomba BEFORWARD kumpatia gari la kubebea wagonjwa
kutokana na mradi wake alioubuni wa kusaidia mama wajawazito vijijini.
Aidha
HINGI ameongeza kuwa baada ya kujibu swali la BEFORWARD walijitokeza
watu wengi waliolipenda wazo lake kwa kuandika ‘like’ na hatimaye
kuibuka mshindi.HINGI amesema atalitumia gari hilo kubebeea wagonjwa katika mradi huo waliouanzisha mkoani MWANZA

0 comments:
Post a Comment