JUMA NATURE AKANA MADAI YA KUMPONDA DIAMOND KWENYE NYIMBO YAKE MPYA…ADAI ‘DADA MONDI’ NI MSANII TOFAUTI.



Hatimaye Juma Nature, amezungumzia utata ulioibuka kwenye wimbo wake mpya Kama Jana, unaohusiana na kama kweli amemdiss Diamond.
 
Akiongea na kipindi cha Showtime Next Chapter, Juma Nature aka Kiroboto amesema jina la ‘Dada Mondi’ lililofanya wengi waamini kuwa ni version yake ya Diamond, ni jina la msanii mwingine kabisa.
 
  “Hamna diss ya kumdiss Diamond, Diamond   hajadisiwa,” amesema Nature  na  kuongeza:
 
  “Pale katajwa mtu mwingine kabisa anaitwa Dada Mondi na anakaa mitaa ya kwetu. Bado hajatoka halafu anataka sifa.”


TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

Post a Comment

Ungana Nasi, Like Page Yetu Hapa Chini