USALITI HAUNA NGUVU SHETANI WA USALITI NI AKILI ILIYOKOSA MALENGO-5

Makala yetu inajieleza kwa kichwa chake hapo juu. Nilishafafanua kinagaubaga jinsi ambavyo usaliti usivyo na nguvu, isipokuwa akili iliyokosa malengo ndiyo inaweza kutenda dhambi hiyo.
Katika kufundisha kwa mifano, nakuletea mfululizo wa mkasa wa Lauryn ambaye ni mke wa mtu, alipojikuta anasaliti ndoa yake kwa kutoka kimapenzi na kijana Paul ambaye ni mpangaji mwenzake.

Nikukumbushe alipokomea hapa; “Nilipotoka chumbani kwa Paul nilikwenda moja kwa moja chumbani kwangu nikiwa na mawazo sana. Nilijisikia vibaya kwa jinsi nilivyokaa uchi mbele ya Paul ambaye kiumri mimi ni mkubwa halafu hatukufanya chochote. Kwa kifupi sioni kitu ambacho hakukiona kutoka kwenye mwili wangu.
Sasa endelea kuusoma mkasa wa Lauryn: “Nasisitiza nilibaki na kabati tu, zaidi ya hapo sikuwa na nguo yoyote, nilijilaumu sana. Kule chumbani kwangu nilitumia muda mwingi kumuwaza Paul, mara nyingi niliona bora angenichokoza ili tukamilishe ngwe. Kuna wakati nilitamani nimrudie chumbani kwake na kumvamia ili tufanye kweli.
“Kilichonifanya nipingane na uamuzi huo ni jawabu kuwa wanaume ni viumbe vuguvugu, kwa maana kama mwanamke ameweka msimamo wake, yeye anakuwa wa moto kumfukuzia ili ampate na pale mwanamke anapojilainisha, mwanaume huwa wa baridi akijifanya hataki kumbe anataka.
“Nikajituliza lakini kuanzia hapo nilianza mitego ya maana. Kosa kubwa ambalo Paul alizoea kulifanya ni kupenda kunizomea, tukawa tunazomeana. Tulipozomeana, tulikuwa tunasogeleana mpaka kugusanisha mapaji ya uso, sijui kwa nini tulifikia hatua hiyo, mpaka leo huwa najiuliza lakini jibu sipati.
“Katika mwendo huo, siku moja usiku tukiwa sebuleni mimi na Paul, huku mume wangu akiwa chumbani amelala kama kawaida yake, kuna kitu alizungumza akakosea, mimi nikamzomea nikamfuata pale alipokuwa ameketi, nikamzomea kwa kugusanisha paji lake la uso na langu.
“Baadaye katika mazungumzo, nami nilikosea, wakati huo nilikuwa nimelala chali kwenye sofa, basi alinifuata kunizomea, paji langu la uso na lake, vikawa vinagusana, kwa maana hiyo midomo inakuwa karibu. Nikamwambia aniache vinginevyo nitamg’ata mdomo. Akaendelea kunizomea na kusababisha tufike hatua mbaya sana katika historia yangu ya usaliti katika ndoa.”
HATUA GANI HIYO?
“Ni wazi kwamba siku hiyo Paul alikuwa katika wakati mgumu zaidi kuliko mimi. Nami hisia zangu zilikuwa motomoto ila kiukweli yeye alinizidi. Sababu ya kusema hivyo ni kwamba nilipomwambia nitamg’ata mdomo, yeye badala ya kushtuka na kuacha, aliendelea..
“Inawezekana alitamani hicho kitendo cha mimi kumg’ata mdomo, maana aliendelea kunizomea huku akiwa amegusisha paji lake la uso kwenye la kwangu. Kwa maana hiyo ule mbadilishano wa pumzi uliendelea. Ilihitaji binadamu mwenye uwezo wa kinabii hasa ili kuyaepuka yale majaribu.
“Nilijifikiria kama mara mbili au tatu, nikajiona nipo sahihi, kwa hiyo Paul alipoendelea kunizomea, mimi nilimng’ata. Niliung’ata mdomo wake wa juu. Si kwamba niliung’ata kwa nguvu mpaka akaumia, la hasha! Nilimng’ata kishkaji, yaani ile danganya toto, nadhani hata yeye alijua nisingemng’ata mpaka akaumia ndiyo maana hakuogopa.
“Kwa takriban nusu dakika, niliung’ang’ania mdomo wake, huku yeye akiwa ametulia akisikilizia. Ilipofikia hatua hiyo, ikawa hakuna mwenye uwezo wa kuzungumza, isipokuwa midomo yetu ndiyo iliwasiliana kwa ukaribu zaidi. Hapo nikawa natamani na yeye aung’ate mdomo wangu wa chini ili twende sawa.
 “Paul hakufanya hivyo, yeye alikwenda hatua moja mbele. Shetani ana nguvu ya ajabu, maana siku hiyo nilikifurahia na kukipongeza mno kitendo cha Paul. Nikiwa natajarajia ananing’ata mdomo wa chini ili kulipa kisasi, yaani mimi niwe namng’ata wa juu, yeye wa chini, Paul hakutumia meno.
“Alitumia ulimi. Akaanza kwa kunilamba mdomo wa chini, mwanzoni niliona kama hisia zangu zinanidanganya kwa sababu alilamba taratibu mno. Baada ya muda ikawa kila kitu dhahiri. Akawa halambi tena, bali alifyonza kama siyo kunyonya. Sisemi uongo, almanusura nipige kelele kwa raha nilizosikia.
“Sisemi uongo, siku hiyo ndiyo nilikuwa napokea kwa mara ya kwanza kiss la nje ya ndoa, tangu nilipoolewa na mume wangu. Sijui kama alibahatisha au ni ufundi aliojaliwa, maana aliufyonza kitaalamu ule mdomo wangu wa chini, mpaka nikapatwa na mchecheto. Kama ingekuwa chumbani, pengine ningemsukuma na kuchojoa viwalo vyote ili tuikamilishe mechi.
“Nilishindwa kufanya hivyo kwa sababu pale tulikuwa sebuleni halafu mume wangu alikuwa chumbani, kwa hiyo hakuwa na kizuizi chochote cha kutoka na kutufumania. Uoga huo ndiyo ulionifanya niidhibiti mizimu yangu ambayo kwa hakika, ilikuwa inaninyevuanyevua ile mbaya.

Itaendelea wiki ijayo.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

Post a Comment

Ungana Nasi, Like Page Yetu Hapa Chini