Rais
mstaafu wa awamu ya sita wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt.
Amani Abeid Karume amesema majumba ya Mpapa yaliyokabidhiwa kwa wananchi
24 kutoka shehia 6 ya jimbo la bambi yanahitaji kulindwa na kutunzwa
ili yaweze kudumu zaidi uhai wake.
Hayo
ameyasema huko bambi wakati alipokua akiyakabidhi nyumba hizo kwa
familia kadhaa katika sherehe za kuzifungua nyumba hizo kwa wakazi
waliopewa,ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha miaka 50 ya Mapinduzi ya
Zanbar.
Amesema
azma ya awali ya mapinduzi ya Zanzibar ni kumpatia makazi bora
mwananchi wa Zanzibar na hiyo ndio iliokuwa azma ya Rais wa awamu ya
kwaza,Hayati Abeid Aman Karume ya kuwajengea wananchi wake makazi
hayo,hivyo azma hiyo ipo palepale na serikali haitorudi nyuma.
Amesema
ujenzi wa nyumba hizo,umemalizika na kuazia leo ni huru kwa wananchi
kuzitumia kwa kuweka familia zao. Sambamba na kuyatunza kwa ubora.
Nae
Waziri wa Ardhi,Maji,Ujenzi na Nishati wa Zanzibar,Mh. Ramadhani Abdalla
Shaban amesema wameshapitisha maamuzi ya kuazisha Shirika la Nyumba
ambalo litasimamia ujenzi na ukarabati wa nyumba zote na maendeleo yake
kwa kushirikiana na wakazi wanao ishi kwenye nyumba hizo.
Aidha
akijibu maombi ya wana kijiji wa Mpapa kuhusiana na tatizo la maji
katika nyumba hizo,amesema zitapatiwa maji si muda mrefu,tatizo la maji
Mpapa litakuwa historia kwa kushirikiana na Mbunge na mwakilishi wa
jimbo hilo.
0 comments:
Post a Comment